Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Rais Samia amfariji mjane wa Magufuli
Habari

Rais Samia amfariji mjane wa Magufuli

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, amekwenda kuifariji familia ya aliyekuwa Rais wa Taifa hilo, Dk. John Pombe Magufuli, jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu

Mama Samia amekwenda kutoa mkono wa pole leo Ijumaa tarehe 19 Machi 2021, mara baada ya kuapishwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma, kuwa Rais wa sita wa Tanzania.

Amechukua nafasi ya Dk. Magufuli, alifikwa na mauti Jumatano tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Makumbusho mkoani Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu ya mfumo wa umeme wa moyo wake.

Mama Samia amemfariji Janeth, mjane wa Dk. Magufuli na binti yake ambapo alipata fursa kuomba dua.

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiongoza sala ya kumuombea aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati John Mgufuli, akiwa sambamba na mtoto wa marehemu pamoja na katibu mkuu kiongozi Dkt. Bashiru Ally

Mama Samia alikuwa ameongozana na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Bashiru Ally.

Mara baada ya kutoka kuifariji familia, Mama Samia alikwenda kusaini kitabu cha kumbukumbu ya maombolezo ya kifo cha Hayati Magufuli (61), katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akisaini kitabu cha maombolezo kwenye viwanja vya Karimjee Dar es Salaam

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari

Serikali yataka vijana  wajiunge na program atamizi ya biashara CBE

Spread the love  SERIKALI imewahamasisha vijana kujiunga na program atamizi inayotolewa na...

AfyaHabari

Ugonjwa wa ajabu ulioua watano Bukoka ni Marburg

Spread the loveWAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu amesema ugonjwa wa ajabu uliosababisha...

AfyaHabariHabari

Ugonjwa wa ajabu wadaiwa kuua watano Kagera, Serikali yatoa tahadhari

Spread the loveJUMLA ya watu watano wanaidaiwa kufariki dunia  katika vijiji vya...

ElimuHabari

CBE yaanzisha Shahada 10 za Uzamili, CBE yajivunia wahitimu wanaoajirika

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimewataka wenye  kampuni na...

error: Content is protected !!