Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia akemea mawaziri walioajiri maafisa habari binafsi
Habari za Siasa

Rais Samia akemea mawaziri walioajiri maafisa habari binafsi

Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan ameonesha kutoridhika na kitendo cha baadhi ya Mawaziri kuajiri maafisa habari binafsi kwaajili ya kuripoti habari zao na si za Serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Rais Samia amesema hayo yanafanyika licha ya kila wizara kuwa na kitengo cha mawasilino sambamba na watumishi wa Serikali.

Mkuu huyo wan chi ameyasema hay oleo Alhamisi tarehe 2 Machi 2023 wakati akifungua semina elekezi kwa mawaziri, naibu mawaziri, makatibu wakuu na naibu makatibu wakuu, inayofanyika jijini Arusha.

“Najua kila wizara ina kitengo cha habari, vitengo hivi vinatumikaje?, vipo tu vimekaa havifanyi kazi lakini bado baadhi yenu Mawaziri mmeajiri maafisa wenu binafsi wa habari wa kutoa taarifa zenu na sio taarifa za Serikali,” amesema Rais Samia na kuongeza;

“Sasa mambo kama haya twende tukarekebishe na nimatumaini yangu kuwa mada kuhusu suala hili litatukumbusha wajibu wetu huo kama viongozi na wasemaji wakuu wa wizara zetu.”

Viongozi hao wakuu wa wizara wanapewa semina hiyo nikiwa ni siku chache tangu Rais Samia kufanya mabadiliko ya baadhi ya wizara kwa kile alichoeleza ni kutoelewana miongoni mwao hivyo kuhitaji kupewa maelekezo ya namna ya utendaji kazi wao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!