Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia akanusha taarifa kwamba alikuwa haelewani na Magufuli
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia akanusha taarifa kwamba alikuwa haelewani na Magufuli

Spread the love

RAIS Samia amesema alinukuliwa vibaya na vyombo vya Habari vilivyosema kwamba alisema hakuwa na maelewano mazuri na Rais John Magufuli kipindi yeye akiwa Makamu wa Rais. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Rais ametoa ufafanuzi huo katika mahojiano na kituo cha UTV yaliyorushwa leo Jumatano tarehe 4 Mei 2022 baada ya kuhojiwa na Mkurugenzi mwendeshaji wa Azam Media, Todi Mhando kuhusu ukweli wa taarifa hiyo.

“Kama walinikuu hivyo basi walikosea, unakuaje makamu wa rais halafu usiwe karibu na rais na hilo ndiyo swali limeshajijibu hivyo,”

Mbali na hayo Rais Samia amesema amejifunza kutoka kwa Rais John Magufuli kusimamia nidhamu ya kazi “lakini pili kuwe na tija katika kufanya kazi na ndiyo maana marehemu (Rais Magufuli) alikuwa mkali sana kutaka kuona matokeo ya kinachofanywa kwahiyo kile na mimi kilinipa mafunzo sana.”

Amesema ukali unaweza kuwa wa maneno na unaweza kuwa wa matendo na kukiri kuwa yeye hana ukali wa maneno, “lakini kwa matendo mtu unaweza kufanya kitu mtu anakuelewa mama amekusudia kuzungumza kitu.”

Vilevile amezungumzia miradi iliyoachwa na mtangulizi wake na kufafanua kuwa hiyo ni miradi yao na si ya Rais Magufuli kwani naye alikuwepo katika Serikali iliyoianzisha.

John Magufuli, Mgombea Urais na Mgombea mwenza wake, Samia Suluhu wakirudisha fomu za kugombea urais

Rais Samia amesema miradi yote waliyoanzisha awamu ya tano ina maana kubwa kwenye wimbi la nne la mapinduzi ya viwanda, “tunapozungumza biashara huru ndani ya Afrika maana yake ni kuwa na njia za usafiri, muwe na reli, muwe na bandari, muwe na barabara na muwe na umeme wa kutosha hata kuuza kwa wengine.”

Alisema changamoto kubwa ni ukubwa wa miradi na uwezo wa ndani wa nchi “ile miradi tulikuwa tunaiendesha kwa mikopo na kwa wakati ule mikopo ambayo tulikuwa tunaipata na hali ya maradhi na kwamba mashirika ya kimataifa ya fedha yalishatengeneza mipango yake kwamba kwa Tanzania tutaoa pesa mwaka huu hizi na hizi kwahiyo miradi haikupata nafasi kwa mwaka ule.”

Alifafanua zaidi kuwa ni sahihi kusema tumejenga kwa fedha zetu kwasababu ni mikopo ambayo itarudishwa kwa wakopeshaji.
“Kama nakuambia nikopeshe nitakulipa ile pesa ni yangu kwasababu nitakulipa kwahiyo tulijenga kwa pesa zetu lakini kwa kukopa. Kwahiyo tatizo ni itaendeleaje lakini nashukuru Mungu.”

1 Comment

  • Fedha za mikopo ni fedha zetu?? Du ya mwaka hiyo. Tuwe wakweli jamani tusizinguane

    Kama ulikuwa unaelewana na JPM mbona ulisema vingine huko ughaibuni? tena imo katika video si uzushi !!!

    Nanyi wanahabari msiwe wanafiki na waoga

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

error: Content is protected !!