Saturday , 3 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia aibeba tena Yanga, aahidi 20 milioni kwa goli la ushindi
Habari Mchanganyiko

Rais Samia aibeba tena Yanga, aahidi 20 milioni kwa goli la ushindi

Spread the love

RAIS Dk.Samia Suluhu Hassan ameibeba tena klabu ya Yanga baada ya kutangaza dau nono la Sh 20 milioni katika mechi za fainali ya Kombe la Shirikisho itakayopigwa tarehe 28 Mei 2023 na marudiano tarehe 3 Juni 2023.

Rais Samia amesema kila bao la ushindi atalipa Sh. 20 milioni lakini pia atatoa ndege ya serikali kuipeleka timu hiyo nchini Algeria kwa ajili ya kumenyana na wapinzani wao USM Alger. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Timu mbili hizo zinatarajiwa kukwaana katika mechi mbili za fainali ya Kombe la Shirikisho, mechi inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa Yanga na Watanzania kwa ujumla kuishuhudia ikiweka historia ya kutwaa taji hilo linaloratibiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).

Akizungumza katika tukio la uzinduzi wa Mradi wa Minara ya kurusha matangazo ya Televisheni ardhini (DTT) ya Kampuni ya Azam, Rais Samia alisema uamuzi huo unatokana na matamanio yake ya kuona timu ya Tanzania inafanya vizuri katika michuano hiyo mikubwa barani Afrika.

“Nilianza kwa kutoa Sh. tano milioni kila goli kwa timu ya Simba na Yanga kwenye michuano hii, lakini pia nikatoa Sh. 10 milioni kila goli moja ambapo bahati mbaya Simba wao wameishia njiani na kuwaacha wenzao Yanga.

Uamuzi wa Rais Samia kutoa mamilioni kwa timu za Simba na Yanga umechangia kwa kiasi kikubwa kuzipaisha timu hizo sambamba na kutangaza soka la Tanzania, ambapo Yanga kwa mara ya kwanza ikifanikiwa kufuzu hatua ya fainali ya Kombe la Shirikisho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Magunia 731 ya bangi yakamatwa, mamia ya hekari yateketezwa Arumeru

Spread the love  MAMIA ya magunia ya madawa ya kulevya aina ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

error: Content is protected !!