Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ahimiza wananchi kuendeleza juhudi za kilimo
Habari za Siasa

Rais Samia ahimiza wananchi kuendeleza juhudi za kilimo

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewahimiza wananchi kuendeleza juhudi katika kilimo kwani Seerikali imechukua hatua za kukuza kilimo nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Manyara … (endelea).

Mkuu huyo wa nchi ameyasema hayo leo Jumatano tarehe 23, Novemba, 2022, wakati akizungumza na wananchi wa mkoa wa Manyara amabo ameutaja kama miongoni mwa mikoa inayotegemewa kwa kilimo nchini.

Rais Samia amesema uzalishaji wa chakula kwa mwaka 2021 ndani ya mkoa wa Manyara ulizalisha ziada ya tani 264,819 ambazo ziliuzwa nje ya mkoa.

“Sasa mkiongeza jitihada zaidi mtazalisha zaidi ya hizi na nasema hivi kwasababu tumeanza kujenga maghala na vihenge ambavyo vinakwenda kuchukua tani nyingi za chakula,” amesema.

Amesema anahimiza kilimo kwasababu miaka ijayo dunia itakuwa na hatari ya njaa na kwamba Tanzania haina sababu ya kulia njaa.

Amesema wanachukua hatua kwa kuweka miundombinu ya mbolea, umwagiliaji, kuanza kilimo cha mashamba makubwa ili chakula kiwe kingi cha kuweka akiba na kuuza kwa majirani.

“Tanzania Mungu ametupendelea ardhi, nzuri, maji tunayo, mvua zinanyesha kwa wakati wake la maana ni kkinga maji na kuyahidhi yatumike kwenye kilimo na matumizi mengine,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!