Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia agoma kuingilia sakata la kina Mdee
Habari za Siasa

Rais Samia agoma kuingilia sakata la kina Mdee

Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan, amekataa kukubali ombi la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuingilia kati sakatala la wabunge viti maalum 19, wanaodaiwa kuwepo bungeni kinyume cha sheria, akisema suala hilo liko mahakamani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

Msimamo huo wa Rais Samia ulitolewa leo tarehe 8 Machi 2023, akizungumza katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani mkoani Kilimanjaro, yaliyoandaliwa na Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha).

Ni baada ya baraza hilo na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, kumuomba aingilie kati ili wabunge hao waondolewe bungeni kwa madai kuwa hakijawateua.

“La mwisho kwa jina mliloliita (Covid-19), wote wawili wamesema japo kwamba lipo mahakamani lakini mama…, niwaambie tuache mkondo ule uendelee tutazame mbele yanayokuja. Tuachie mkondo ule uendelee, si rahisi mimi hata kama ni Rais kutia mkono huko,” amesema Rais Samia.

https://www.youtube.com/watch?v=RtdYO5O0tXk&t=33s

Wabunge hao wakiongozwa na Halima Mdee, walifungua kesi Na. 36/2022 katika Mahakama Kuu, Masjala Kuu, jijini Dar es Salaam, kupinga uamuzi wa Chadema kuwavua uanachama kwa tuhuma za usaliti kufuatia uamuzi wao wa kwenda kuapishwa bungeni jijini Dodoma, kuwa wabunge viti maalum.

Katika kesi hiyo inayosikiliwa mbele ya Jaji Cyprina Mkeha, Mdee na wenzake wanadai hawakujipeleka bungeni, bali waliteuliwa na uongozi wa chama hicho, hivyo wanaiomba mahakama ifanye mapitio dhidi ya mchakato uliotumika kuwavua uanachama wakidai haukuwa halali.

Kwa sasa kesi hiyo inaendelea kusikilizwa mahakamani hapo, ambapo kesho tarehe 9 Machi 2023, mawakili wao wataanza kuwahoji baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wadhamini la Chadema, akiwemo Dk. Azaveli Lwaitama, dhidi ya hati zao za viapo kinzani walizowasilisha mahakamani kujibu malalamiko ya wabunge hao kufukuzwa kinyume cha sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!