Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia afanya uteuzi, Anne Makinda…
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia afanya uteuzi, Anne Makinda…

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa wenyeviti wanne wa  Bodi za Wakurugenzi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Taarifa iliyotolewa na Jaffar Haniu, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu imesema, uteuzi wa wenyeviti hao, umefanyika leo Jumatano, tarehe 16 Juni 2021.

Amewataja walioteuliwa ni;

1. Juma Alli Mohamed Muhimbi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.

Kabla ya uteuzi huo, Muhimbi alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Transparent Finacial and Tax Consulting Services Ltd ya Dar es Salaam.

Muhimbi anachukua nafasi ya Mama Anne Makinda, Spika mstaafu wa Bunge la Tanzania, ambaye muda wake umemalizika.

2. Amemteua Dk. EdmundMndolwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Posta Tanzania (TPB).

Dk. Mndolwa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), anaendelea na wadhifa huo baada ya kumaliza kipindi chake cha kwanza.

3. Amemteua Prof. John Wajanga Aron Kondoro kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Prof. Kondoro anaendelea na wadhifa huo baada ya kumaliza kipindi chake cha kwanza.

4. Aidha, Rais Samia amemteua Prof. Valerian Cosmas Kanyengele Silayo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC).

Prof. Silayo ni Profesa wa Chuo Kikuu cha Kilimo Morogoro (SUA).

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

Habari Mchanganyiko

TPF-NET Arusha yaonya jamii ya wafugaji zinazoendeleza ukatili wa watoto na wanawake

Spread the love  MTANDAO wa Polisi wanawake wa Arusha kuelekea siku 12...

Habari Mchanganyiko

Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Greyhorse zasaini mkataba wa bil.7.4

Spread the loveTAASISI ya Mwalimu Nyerere (MNF) imesaini mkataba wa miaka 10...

error: Content is protected !!