
Bweni la Shule ya Sekondari ya Kiislam ya Wasichana AT TOWN likiteketea kwa moto
SAMIA Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kwa kushirikiana na Jumuiya za Kiislamu Tanzania kutafuta chanzo cha matukio ya moto yanayojitokeza kwenye shule zinazomilikiwa na Waislamu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Rais Samia ametoa maagizo hayo, leo Jumapili tarehe 11 Julai 2021, ikiwa ni siku moja imepita tangu moto ambao haujajulikana chanzo chake, kuteketeza Bweni la Shule ya Sekondari ya Kiislam ya Wasichana AT TOWN, iliyopo mji mpya, mkoani Morogoro.
Moto huo, uliibuka jana usiku Jumamosi, umetekeleza mara mbalimbali kama vitanda, magodoro, madaftari na vitabu.
Soma zaidi:-
Moto soko la Kariakoo, Rais Samia atoa pole, maagizo
Taarifa ya Jaffar Haniu, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, imemnukuu Rais Samia akitoa pole kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Martin Shigella na Jumuiya za Kiislaam Tanzania kufuatia kuungua moto kwa Bweni hilo.
Rais Samia amesema kumekuwa na matukio ya mara kwa mara ya kuungua moto kwa shule zinazomilikiwa na Jumuiya za dini nchini.
Kutokana na hilo, Rais Samia ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kwa kushirikiana na Jumuiya hizo kutafuta vyanzo vya matukio hayo na kuyadhibiti ili matukio ya kuungua moto kwa shule hizo yasijirudie.
More Stories
Huduma ya Teleza Kidigitali yazinduliwa Morogoro
Taasisi yaanzisha mafunzo kuwanoa wadau wa mawasiliano nchini
GGML yatoa msaada wa magari manne VETA Mwanza