Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia aagiza mikataba ujenzi wa miundombinu isainiwe hadharani
Habari za Siasa

Rais Samia aagiza mikataba ujenzi wa miundombinu isainiwe hadharani

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

WAZIRI wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amesema Rais Samia Suluhu Hassan ameagiza mikataba ya ujenzi wa miundombinu ya barabara iasainiwe hadahrani ili wananchi waweze kushuhudia na kufuatilia utekelezaji wake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea).

Mbarawa amebainisha hayo leo Jumanne tarehe 27 Desemba, 2022, wakati wa utiliaji saini mkataba wa ujenzi wa barabara tatu zenye jumla ya kilomita 32 zilizopo Kyela Mkoani Mbeya.

Mbarawa amesema Rais alimhoji sababu ya Wakala wa Barabara Tanzania TANROADS, kusaini mikataba ya ujenzi wa miundombinu ndani na kuagiza kuanzia sasa mikataba hiyo isainiwe hadharani

“Mheshimiwa Rais aliniuliza kwanini TANROADS wanakuwa na utaratibu wa kujifungia kwenye chumba wanasaini miradi, akasema kwaajili ya mradi huu nendeni Kyela mkasaini mradi huu mbele ya wananchi wote washuhudie,” amesema Mbarawa.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera amempongeza Rais Samia kwa kutoa maagizo hayo.

“Watanzania lazima wajue, hii mikataba siku zote huwa inasainiwa makao makuu ya TANROADS, leo hii kwa mara ya kwanza toka nchi hii izaliwe tunasaini mikataba hadharani ili wananchi waweze kujua mikataba hii imesainiwa…ili muone Mheshimiwa Rais barabara hii anakuja kuijenga,” amesema Homera.

Ujenzi wa kilomita 32 utahusisha Barabara ya Ibanda-Kajunjumele kilomita 22, Kajunjumele-Kiwara Port kilomita 6, Kajunjumele-Itungi Port kilomita 4 kwa kiwango cha lami. Barabara hizio zitaunganisha mkoa wa Mbeya na mikoa ya Ruvuma na Njombe kupitia ziwa Nyasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!