Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari Rais Ramaphosa ataja siri Magufuli kutosafiri nje
Habari

Rais Ramaphosa ataja siri Magufuli kutosafiri nje

Cyril Ramaphosa, Rais wa Afrika Kusini
Spread the love

 

RAIS wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa amesema, aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, alimwambia hapendi kusafiri nje ya nchi, kwa kuwa alitaka kupata muda wa kutosha kuwatumikia Watanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Kiongozi huyo wa Afrika Kusini, ametoa kauli hiyo leo Jumatatu tarehe 22 Machi 2021, katika mazishi ya kitaifa ya Hayati Magufuli, iliyofanyika makao makuu ya nchi, jijini Dodoma.

Akielezea historia ya Hayati Magufuli, Rais Ramaphosa amesema, awali alidhani mawanasiasa huyo anaogopa kupanda ndege, lakini baadaye alifahamu kwamba alibaki Tanzania kuwatumikia wananchi wake.

“Magufuli alikuwa sio msafiri mkubwa, alikuwa hapendi kusafiri. Alipenda kubaki nyumbani, nilidhani alikuwa anaogopa kusafiri kwenye ndege, lakini aliniambia alibaki hapa kuendelea kuwatumikia Watanzania badala ya kutembelea nchi za nje,” amesema Rais Ramaphosa.

Rais Ramaphosa amesema Hayati Rais Magufuli alimueleza siri hiyo alipokwenda Afrika Kusini, kushuhudia sherehe yake ya kuapishwa kuwa Rais wa taifa hilo kusini mwa Afrika.

Mwanasiasa huyo aliyeapishwa Februari 2018 kuwa Rais wa Afrika Kusini, amesema ujio wa Hayati Rais Magufuli nchini humo, ulimfanya ajisikie anaheshimiwa.

Hayati Rais Magufuli alifariki dunia tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Makumbusho mkoani Dar es Salaam, alikokuwa anapatiwa matibabu ya matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo.

Mwili wake unatarajiwa kuzikwa kijijini kwao Chato mkoani Geita, Ijumaa tarehe 26 Machi 2021.

Hadi umauti unamkuta, Hayati Magufuli hakuwa na desturi ya kusafiri nje ya nchi na hakuwahi kusafiri kwenda nje ya Afrika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!