Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Mwinyi: Huu ni msiba mzito
Habari za Siasa

Rais Mwinyi: Huu ni msiba mzito

Spread the love

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, ametoa salamu za rambirambi kwa Mama Janeth Magufuli, familia pamoja na Makamu wa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan na wananchi wote wa Tanzania kufuatia kifo cha Rais wa taifa hilo, Dk. John Pombe Magufuli. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea)

Katika salamu hizo za rambirambi, Rais Mwinyi, amesema, amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli kilichotokea jana Jumatano tarehe 17 Machi 2021, mkoani Dar-es-Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Salamu hizo za Rais Mwinyi, zimeeleza, huu ni msiba mzito sana kwake na kwa taifa la Tanzania, hivyo aliwaomba wananchi kuwa na subira na utulivu katika kipindi hichi kigumu cha msiba huu mzito wa kitaifa.

Kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na wananchi wote wa Zanzibar, Rais Mwinyi alitoa salamu hizo za rambirambi na kumuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu mahala pema peponi, Amin.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

Habari za Siasa

Alichokisema Rais Samia baada ya kupokea ripoti ya CAG, TAKUKURU

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake itafanyia kazi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

error: Content is protected !!