Tuesday , 26 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani
Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar
Spread the love

 

RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein Ally Mwinyi, amezindua Kamati ya Maridhiano Visiwani, yenye lengo la kuendeleza dhamira ya kushirikiana na kuimarisha Umoja wa Kitaifa Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Halfa ya uzinduzi huo, imefanyika leo, Ikulu mjini Unguja, ambapo Rais Mwinyi, alitumia fursa hiyo, kumshukuru Rais wa Jamhuri na mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan, kwa kumridhia kukutana na kufanya mazungumzo na viongozi wakuu wa chama cha ACT- Wazalendo.

Katika hafla hiyo, iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali, wakiwamo Juma Duni Haji, Mwenyekiti wa taifa wa ACT – Wazalendo; Zitto Zuberi Kabwe, Kiongozi Mkuu wa chama hicho na Othman Masoud Othman, makamu mwenyekiti wake Zanzibar na Makamu wa Kwanza wa Rais Visiwani.

Wengine, ni Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) ya CCM na Makamu wa Pili wa Rais, Hemed Suleiman Abdullah, pamoja na viongozi wengine mbalimbali wa chama hicho Visiwani.

Juma Duni Haji, Naibu Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo

Dk. Mwinyi alimshukuru Rais wa Samia kwa uamuzi wake wa kufanya vikao na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na kusikiliza maoni yao, ambayo amesema “yameendelea kuyafanyiwa kazi na kutekeleza kwa vitendo azma ya kuleta maridhiano ya kisiasa ikiwemo kuunda Kikosi Kazi, kilichopitia ripoti ya Baraza la Vyama vya Siasa nchini.

Aidha, Dk. Mwinyi alisema, rais Samia ameimarisha uhuru wa kisiasa na kidemokrasia kwa kuruhusu tena kufanyika kwa mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa, na kuanzisha mchakato wa Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano.

Amesema, hotuba yake aliyoitoa Novemba 2020 wakati anazindua Baraza la Wawakilishi, kwamba dhamira yake ni kuwaunganisha wananchi wote wa Zanzibar kuwa wamoja, bila kujali rangi, asili, imani za dini au itikadi za kisiasa, yaweza kuthibitishwa na kitendo chake hicho.

Dk. Mwinyi alisema, “dhamira ya kuiendeleza Zanzibar, ni jukumu la kila mmoja.”

Hata hivyo, taarifa iliyotolewa na Ikulu ya Zanzibar, leo Jumatano, tarehe 31 Mei 2023, haikutaja majina ya wajumbe wa Kamati ya Maridhiano ambayo rais Mwinyi ameripotiwa kuizundua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

Habari za SiasaTangulizi

Chande aliyeng’olewa TANESCO kwenda TTCL apelekwa Posta

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa, Mkurugenzi Mkuu wa...

Habari za Siasa

Kamugisha aanika utekelezaji mpango kazi 2022/23

Spread the loveMWENYEKITI wa Ngome ya Vijana ya Chama Cha ACT-Wazalendo Mkoa...

Habari za Siasa

Vijana ACT-Wazalendo wakabidhiwa kivumbi kulinda kura uchaguzi 2024,2025

Spread the loveNGOME ya Vijana ya Chama cha  ACT-Wazalendo, imetakiwa kuwanoa wafuasi...

error: Content is protected !!