Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Mwinyi ateua wakurugenzi wanne, yumo wa ZEC
Habari za Siasa

Rais Mwinyi ateua wakurugenzi wanne, yumo wa ZEC

Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar
Spread the love

 

RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi, ameteua wakurugenzi wanne, akiwemo Khamis Kona Khamis, aliyemteua kuwa Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi visiwani humo (ZEC). Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo Ijumaa, tarehe 16 Julai 2021 na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar, Mhandisi Zena Said.

“Rais Mwinyi amefanya uteuzi wa wakurugenzi, Khamis Kona Khamis ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar,” imesema taarifa ya Mhandisi Zena.

Khamis anachukua nafasi ya Thabit Idarous Faina, ambaye ameondolewa katika nafasi hiyo na Rais Mwinyi.

Mbali na uteuzi wa mkurugenzi wa ZEC, Rais Mwinyi amemteua Mohamed Ame Makame, kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar.

Pia, amemteua Said Mtumwa Faki, kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Serikali wa Uchapaji na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali visiwani humo (ZAGPA).

“Bibi Mshauri Khamis Abdulla, ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mipango ya Rasilimali Watu, katika Ofisi ya Rais, Sheria, Utumishi na Utawala Bora. Uteuzi huo unaanzia leo,” imesema taarifa Mhandisi Zena.

1 Comment

  • Hongera hongera Mheshimiwa Rais wa Zanzibar tunashkuru sana unafanya kazi baba Mungu akusaidie tuliomba meter miezi mitatu bila mafanikio leo mafundi wapo hapa wanafunga Mungu akusaidie katika utendaji wako imara thabit

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

error: Content is protected !!