Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari Rais Mwinyi: Asiyekuwemo, hatoingizwa
Habari

Rais Mwinyi: Asiyekuwemo, hatoingizwa

Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar
Spread the love

RAIS wa Zanzibar, Hussein Mwinyi amesema, katika hatua anazochukua kuondoa ‘uchafu’ katika Serikali yake, ‘asiyekuwemo hatoingizwa.’ Anaandika Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kongamao la Jumuiya Tatu za Chama Cha Mapinduzi (CCM), visiwani humo leo Jumatano tarehe 6 Januari 2021, Rais Mwinyi amesema ‘yule atakayekuwemo, atachukuliwa hatua.’

“Kwa hivyo, ombi langu kwenu nyote ni kuunga mkono juhudi za kukabiliana na hali hii,” amesema Rais Mwinyi huku akiungwa mkono na wanakongamano kwa kupiga kelele na vigelegele.

Rais huyo amesisitiza azma yake ya kutofukua makaburi kwa watendaji wabovu waliopita, amesema Watanzania bara na visiwani wameiamini CCM na ndio maana wameipa kura nyingi.

Amesema, hatua zinazochukuliwa na Serikali yake, zinafurahiwa na wengi lakini zinakera wachache huku akisisitiza ‘watuvumilie,’ na kwamba “ili ufanikiwe kulitumbua jibu basi yakupasa kuvumilia maumivu.”

Amewataka viongozi waliochaguliwa kurudi kwa wananchi kutatua shida zao kwa kuwa, baadhi yao huwa na tabia ya kuwasahu wananchi baada ya kuwachagua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!