Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Mwinyi aikabidhi cheti NMB
Habari Mchanganyiko

Rais Mwinyi aikabidhi cheti NMB

Spread the love

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amemkabidhi Afisa mkuu wa Teknolojia na mabadiliko ya kidigitali wa Benki ya NMB, Kwame makundi  cheti cha kushukuru udhamini wa NMB kwenye kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Makabidhiano hayo yalifanyika baada ya mchezo wa fainali ya kombe la Mapinduzi Januari 13, 2023  katika uwanja wa Amaani Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi (watatu kulia) akimkabidhi Afisa mkuu wa Teknolojia na mabadiliko ya kidigitali wa Benki ya NMB, Kwame makundi (kushoto) cheti cha kushukuru udhamini wa Benki ya NMB kwenye kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar. Makabidhiano hayo yalifanyika baada ya mchezo wa fainali ya kombe katika uwanja wa Amaani huko Zanzibar. Kulia ni Naibu waziri wa Utamaduni sanaa na michezo wa Tanzania, Pauline Gekul na wapili kulia na Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdallah.

Katika mchezo huo uliozikutanisha Mlandege FC ya Zanzibar na Singida Big Star’s ilishuhudia dakika 90 zikimalizika kwa Mlandege kulibakisha kombe hilo baada ya ushindi wa 2-1.

Ni mchezo uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Zanzibar na Tanzanka Bara akiwemo  Naibu waziri wa Utamaduni sanaa na michezo, Pauline Gekul.

Pia,  Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdallah alikuwa miongoni mwa walioshuhudia Mlandege ikirejesha tabasamu kwa Wazanzibar lililokuwa limepotea zaidi ya miaka 10.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!