Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais mteule William Ruto kuapishwa Jumanne ijayo
KimataifaTangulizi

Rais mteule William Ruto kuapishwa Jumanne ijayo

Spread the love

RAIS mteule wa Kenya, William Ruto anatarajiwa kuapishwa Jumanne, tarehe 13 Septemba, 2022. Hii ni baada ya Mahakama ya Juu Milimani kutupilia mbali ombi la mpinzani wake Raila Odinga, kutaka ushindi wa Ruto ubatilishwe. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mpangilio wa shughuli utafanyika katika muda wa wiki moja ijayo kabla ya hafla ya kuapishwa kwa Ruto na naibu wake Rigathi Gachagua.

Kwa mujibu wa kifungu cha 141 cha Katiba ya Kenya rais mteule anatakiwa kuapishwa Jumanne ya kwanza baada ya siku saba za mahakama kutoa uamuzi hivyo, kuapishwa kwa rais mteule William Ruto kutafanyika Jumanne ijayo.

Rais mteule huyo atachukua madaraka kwa kula kiapo cha utii na kuapa kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu yake.

Wakati wa hafla hiyo Rais Mteule ataapishwa hadharani mbele ya Jaji Mkuu au Naibu Jaji Mkuu ikiwa Jaji mkuu hayupo.

Baada ya kuapishwa, Rais atatia saini cheti cha kuapishwa na Rais anayemaliza muda wake atamkabidhi Rais zana za mamlaka, upanga na Katiba.

Hayo yanajiri baada ya Mahakama hiyo  jana Jumatatu kuthibitisha kuchaguliwa kwa Ruto kama Rais wa tano wa Jamhuri ya Kenya.

Akisoma uamuzi huo, Jaji Mkuu Martha Koome alisema Ruto alipata asilimia 50 pamoja na kura moja kama inavyohitajika kisheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!