Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Msumbiji awatimua waziri ulinzi, mambo ya ndani
Kimataifa

Rais Msumbiji awatimua waziri ulinzi, mambo ya ndani

Rais wa Msumbiji, Filipe Nyusi
Spread the love

 

RAIS wa Msumbiji, Filipe Nyusi amemfuta kazi Waziri wa ulinzi wa nchi hiyo, Jaime Augusto Neto bila kufafanua sababu halisi za kumchukua uamuzi huo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hatua hiyo imekuja siku moja baada ya rais kumfukuza kazi Waziri wa mambo ya ndani, Amade Miquidade.

Taarifa iliyotolewa jana tarehe 10 Novemba, 2021 na Ofisi ya Rais Ikulu, imeseme Rais amemfuta kazi waziri huyo bila kueleza kwanini amewafuta kazi viongozi wakuu wa ulinzi na usalama wa nchi.

Aidha, inaelezwa kuwa uamuzi huo unahusiana na kuongezeka kwa visa vya utekaji nyara, mauaji, ugaidi na ufisadi, pamoja na kuongezeka kwa idadi ya ajali za barabarani.

Baadhi ya kesi hizo zimehusisha askari wa ulinzi na usalama.

Waangalizi wa mambo ya usalama wamemtaka Rais Nyusi kueleza maamuzi yake ili kuepuka uvumi, hofu na kuibua fujo.

Wanasema si jambo la kawaida kuwatimua viongozi wawili wakuu wa usalama kwa siku chache na kwamba lazima kuwe na sababu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!