Wednesday , 27 September 2023
Home Kitengo Maisha Elimu Rais Mkapa ateuliwa tena kuwa Mkuu wa UDOM
Elimu

Rais Mkapa ateuliwa tena kuwa Mkuu wa UDOM

Spread the love

RAIS John Magufuli amemteua Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). Anaripoti Regina Mkonde … (endelea). 

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo tarehe 14 Mei 2019 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Gerson Msigwa.

Taarifa ya Msigwa inaeleza kuwa, Rais Magufuli amemtea Mkapa kushika wadhifa huo kwa kipindi cha pili mfululizo.

Aidha, Rais Magufuli amemteua Profesa Ignas Rubaratuka kushika wadhifa wa Uwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) kwa kipindi cha pili mfululizo.

“Uteuzi wa viongozi ho umeanza tarehe 10 Mei 2019,” inaeleza sehemu ya taarifa ya Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Elimu

Green Acres kuwakatia bima wanafunzi wote

Spread the loveShule ya Green Acres imejipanga kufanya mambo makubwa kwa mwaka...

Elimu

Vipaji Green Acres vyawafurahisha wazazi

Spread the love WANAFUNZI wa Shule ya Msingi Green Acres, wamewapagawisha wazazi...

ElimuHabari Mchanganyiko

Mtwara Girls waondokana na changamoto ya maji

Spread the love  WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari ya Wasichana mkoani Mtwara...

Elimu

Rc Singida atoa siku 7 kukamilisha miradi elimu ya sekondari

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Singida Peter Selukamba ametoa siku saba...

error: Content is protected !!