Wednesday , 27 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Rais Magufuli uso kwa uso na Mbowe msibani
Habari Mchanganyiko

Rais Magufuli uso kwa uso na Mbowe msibani

Rais John Magufuli alipohani msiba wa Meja Jenerali Alfred Mbowe nyumbani kwake Salasala, Dar es Salaam
Spread the love

RAIS John Magufuli leo tarehe 30 Julai 2019 ametoa salamu za pole kwa familia ya marehemu Meja Jenerali Mstaafu, Alfred Mbowe, aliyefariki dunia tarehe 28 Julai mwaka huu. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Rais Magufuli ametoa salamu hizo alipowasili nyumbani kwa marehemu Jenerali Mbowe, maeneo ya Salasala jijini Dar es Salaam.

Rais Magufuli alipokelewa na Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa ambaye ni mdogo wa marehemu Meja Jen. Mstaafu Mbowe.

“Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli amewasili Salasala jijini Dar es Salaam. Kutoa pole kwa familia kufuatia kifo cha Meja Jen. Mstaafu Alfred Lameck Mbowe,” inaeleza taarifa ya Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari Mchanganyiko

Wizara ya madini kurusha ndege ya utafiti wa madini Geita

Spread the loveKutokana na mchango wa wachimbaji wadogo wa madini kwenye pato...

Habari Mchanganyiko

Jafo aagiza kampuni za madini kuzingatia utunzaji mazingira, azitaka zijifunze kwa GGML

Spread the loveWAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia apewa tano ujenzi barabara Mtwara

Spread the loveWANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk....

error: Content is protected !!