Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Magufuli uso kwa uso na Mbowe msibani
Habari Mchanganyiko

Rais Magufuli uso kwa uso na Mbowe msibani

Rais John Magufuli alipohani msiba wa Meja Jenerali Alfred Mbowe nyumbani kwake Salasala, Dar es Salaam
Spread the love

RAIS John Magufuli leo tarehe 30 Julai 2019 ametoa salamu za pole kwa familia ya marehemu Meja Jenerali Mstaafu, Alfred Mbowe, aliyefariki dunia tarehe 28 Julai mwaka huu. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Rais Magufuli ametoa salamu hizo alipowasili nyumbani kwa marehemu Jenerali Mbowe, maeneo ya Salasala jijini Dar es Salaam.

Rais Magufuli alipokelewa na Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa ambaye ni mdogo wa marehemu Meja Jen. Mstaafu Mbowe.

“Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli amewasili Salasala jijini Dar es Salaam. Kutoa pole kwa familia kufuatia kifo cha Meja Jen. Mstaafu Alfred Lameck Mbowe,” inaeleza taarifa ya Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!