Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli: Nitamkaba Lukuvi alipe pesa zangu
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli: Nitamkaba Lukuvi alipe pesa zangu

Spread the love

RAIS John Magufuli amesema, atamkaba Waziri wa Ardhi, William Lukuvi ili amlipe Sh. 1 milioni fedha alizowapa wazee wawili ambao mmoja wao alidhulumiwa eneo lake. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Rais Magufuli amesema hayo leo tarehe 5 Septemba, 2018 wakati akizungumza na wakazi wa Wilaya ya Bunda mkoani Mara, baada ya kupokea malalamiko ya kuporwa ardhi yaliyotolewa na wazee hayo.

Bibi Nyasasi Masige (mwenye kiwanja) akiwa na jirani yake wamemlalamikia Rais Magufuli kuwa, kuna tajiri aliyedhulimu kiwanja cha mmoja wao baada ya kumuuzia kiwanja cha pili kwa ajili ya kupata fedha za matibabu, na kwamba aliporudi kutoka kupata matibabu alikuta tajiri huyo amejimilikisha kiwanja cha pili.

Wazee hao walidai kuwa, mgogoro wao ulimfikia Waziri Lukuvi ambapo aliagiza bibi huyo kupatiwa kiwanja chake jambo ambalo halijafanyika hadi leo.

Kufuatia malalamiko hayo, Rais Magufuli alimtafuta Waziri Lukuvi kwa njia ya simu, na kumuagiza kumsimamisha kazi kamishna wa ardhi wa kanda hiyo kuanzia leo.

Baada ya hapo Rais Magufuli aliwakabidhi wazee hao kila mmoja Sh. 500,000 kutokana na usumbufu walioupata na kwamba, fedha hizo zitalipwa na Waziri Lukuvi. Rais Magufuli yupo mkoani Mara kwa ziara ya kikazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

error: Content is protected !!