Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli: Nilinyweshwa sumu nife
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli: Nilinyweshwa sumu nife

Rais John Magufuli akizindua kitabu cha Rais Mstaafu, Hayati Benjamin Mkapa, wengine ni wastaafu, Jakaya Kikwete na Ali Hassan Mwinyi
Spread the love

RAIS John Mafufuli ametoa siri yake ya moyoni, namna alivyonusurika kuuawa kwa kunyweshwa sumu, wakati akiwa Naibu Waziri wa Ujenzi wakati wa utawala wa Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa. Anaripoti Martin Kamote … (endelea).

Amesema, kilichomponza ni sifa alizomwagiwa na Rais Mkapa kutokana na uchapa kazi wake, na kwamba jambo hilo hawezi kulisahau.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kitabu cha maisha ya Rais Mkapa kiituwacho ‘Maisha Yangu, Kusudio Langu’ leo tarehe 12 Novemba 2019, katika Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam amesema, baada ya mkasa huo aliomba kujiuzulu.

Tukio la kunyweshwa sumu lilitokea baada ya Rais Mkapa kumtamka kuwa, Rais Magufuli (wakati akiwa waziri) ndiye askari mwavuli wake namba moja.

“Licha ya dhamira njema ya Mzee Mkapa, suala hilo liliniletea mimi matatizo binafsi. Nilianza kuona dalili za baadhi ya mawaziri, tena wengine wa ngazi za juu kabisa kuanza kunichukia.

“Na muda si mrefu, baada ya hapo nikanyweshwa sumu Dodoma, ambayo almanusura iondoe uhai wangu. Lakini kwa neema za Mweneyzi Mungu, nikakiepuka kifo,” amesema Rais Magufuli.

Kutokana na tukio hilo, amesema alikwenda kwa Mzee Mkapa kuomba kujiuzulu “nakumbuka siku hiyo aliniangalia jicho la baba kwa mwana, akinihurumia,” amesema na kuongeza;

“Lakini baada ya dakika chache akaniambia, nanukuu ‘John kafanye kazi, kamtangulize Mungu,’ baada ya hapo nikapewa ulinzi, nikaendelea kuchapa kazi.”

Rais Magufuli amesema, katika tukio hili, alimuona Mzee Mkapa ni mtu anayempa matumaini hata kama mtu amekata tamaa.

“Nimejifunza kutowasifu wateule wangu mimi, hatakama wanafanya kazi vizuri kwasababu yasije yakawapata yale yaliyonipata mimi baada ya wewe kunisifu. Nimeona niliseme hili kwa sababu halijazungumzwa popote,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!