SAFARI ya Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyoanza siku 1670 zilizopita inahitimishwa leo Jumanne tarehe 16 Juni 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea)
Bunge hilo la 11 linaloongozwa na Spika Job Ndugai lilianza safari yake rasmi tarehe 20 Novemba 2015 kwa Rais wa Tanzania, John Magufuli kulizindua.
Siku ya uzinduzi wa Bunge hilo, wabunge wote wa upinzani, wakiongozwa na Freeman Mbowe, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni walitoka ndani ya ukumbi.
Leo Jumanne, Rais Magufuli anakwenda kulihutubia Bunge hilo ili kuruhusu kwenda katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 2020.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI ONLINE & MwanaHALISI TV kwa habari zaidi
Hili ndio Bunge la hovyo zaidi kutokea tangu Uhuru!! Kwa kweli mhimili huo wa dola haujapata kiongozi mahiri tangu kuondoka kwa Mzee Samuel Sitta. Bunge la Sasa lilijikita zaidi katika kujipendekeza kwa rais Magufuli!! Shame of CCM MPs.😬