Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli, Kikwete wateta Ikulu
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli, Kikwete wateta Ikulu

Rais John Magufuli akiwa na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete
Spread the love

RAIS John Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Rais mstaafu wa awamu ya nne, Dk. Jakaya Kikwete leo tarehe 23 Oktoba 2018 Ikulu jijini Dar es Salaam. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa, inaeleza kuwa Rais Magufuli na Dk. Kikwete wamekutana kwa utaratibu wa kawaida wa kusalimiana na kutakiana heri katika majukumu.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa, katika mazungumzo hayo Dk. Kikwete amesifu utendaji kazi wa Rais Magufuli na kumtaka aendelee hivyo hivyo, huku akiahidi kumpa ushirikiano wa hali na mali.

“Nimekuja kumsalimia na kumtakia kila la heri, anafanya kazi nzuri aendelee tu kuchapa kazi na sisi tupo kwa namna yoyote ya kumpa nguvu, tupo tayari kumsaidia,” amesema Dk. Kikwete.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!