Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari Rais Magufuli: Jeshi msikubali vikwazo
HabariHabari Mchanganyiko

Rais Magufuli: Jeshi msikubali vikwazo

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli, Amiri Jeshi Mkuu wa Nchi, ameyataka majeshi nchini kutokubali kuwekewa vikwazo, katika utekelezaji wa majukumu yake. Anaripoti Martin Kamote…(endelea)

Rais Magufuli ametoa wito huo leo tarehe 25 Novemba 2019 wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa, Kikombo, Wilaya ya Chamwino jijini Dodoma.

“Milima yote chukueni ili  mlinde vizuri nchi hii, najua mtaitumia vizuri sababu majeshi ya Tanzania ni imara, msipate vikwazo. Mtu akikaa kule na ng’ombe amewapa vikwazo. Na jeshi halitakiwi kupewa vikwazo, labda vikwazo wakati wa mazoezi, vinavyowafanya kuwa imara, “ amesema Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amesisitiza usalama wa viongozi wa jeshi, na kuwashauri makazi yao yasijulikane hovyo.

“Lazima muelewe vitu vingine lazima viwe vyenu, kama ni nyumba anakaa CDF wengine wasipajue, kama ni nyumba anakaa askari wa jeshi wengine si lazima wapajue.

Ninatambua yale yote mliyokuwa mnayaonesha leo, ni mfano wa mtakayoyafanya sio uhalisia,” ameshauri Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!