Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli awatimua wanunuzi wa Korosho, sasa kununuliwa na Serikali
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli awatimua wanunuzi wa Korosho, sasa kununuliwa na Serikali

Spread the love

RAIS John Magufuli amezikataa kampuni 13 zilizojitokeza kununua korosho ghafi na badala yake ameiagiza Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kutoa fedha za kununua zao hilo, kupitia Jesho la Wananchi (JWTZ). Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 12 Novemba 2018, Rais Magufuli amesema pamoja na makapuni hayo kujitokeza kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, wanaachana na wanunuzi hao kwani watawasumbua, hivyo Serikali itanunua korosho ghafi kwa bei ya Sh. 3,300 kwa kilo, na kuagiza JWTZ) kusimamia mchakato wa ununuzi na usambazaji wa zao hilo.

“Tani 92,000 zimeshanunuliwa, TADB tutanunua kwa 3,300 wakalipwe wakulima kwa kila kilo. Ambayo haijabanguliwa inunuliwe 3,300. JWTZ panga kikosi chako vizuri kila ghala lililoko kule lenye korosho mlinde, jeshi muangalie na walipwe bila kuchelewa, watakapokuwa wanalipwa wasidaiwe chochote, sababu walikuwa wanakopa sio wakakae hapo wakati wanalipwa wawakate hapana,” ameagiza Rais Magufuli.

Rais Magufuli ametoa maagizo hayo baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kueleza kuwa, baada ya serikali kutoa siku nne kwa wanaohitaji kununua zao hilo kujitokeza, kampuni 13 zimejitokeza kununua korosho ghafi.

“Nimeamua yafuatayo, hawa waliojaribu kuleta kwako mapendekezo achana nao hawa watakuja kutuchezea watakwambia wanataka kununua baadae wataanza kuleta masharti na kudelay ‘kuchelewa’ kwa wakulima wetu, wanasema watanunua kwa 3,000 je ikipanda bei ya korosho mwezi wa 12 ‘Desemba, hao wanaoendelea kuja wala wasihangaike kuja, nimeshafunga wala wasihangaike, korosho tunanunua wenyewe,” amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!