Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli awatega wakuu wa wilaya, mikoa
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli awatega wakuu wa wilaya, mikoa

Spread the love

RAIS John Magufuli amewaweka mtegoni Wakuu wa Wilaya na Mikoa walioko katika maeneo yenye migogoro sugu  ya ardhi, akiwataka kusema iwapo wameshindwa kuitatua migogoro hiyo ili awateue wengine. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo tarehe 6 Septemba, 2018 wakati akizungumza na wananchi wa Butiama katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa barabara ya makutano ya Nyamuswa-Sanzate-Nata na Ikoma Gate katika sehemu ya makutano ya Sanzate, iliyofanyika Butiama mkoani Mara.  

“….Ukikaa mahali kukiwa na migogoro mjue mmeshindwa kutawala, kuna polisi, kuna sheria ya ardhi na ya vijiji, mna madaraka haiwezekani mkakaa mahali kukawa na migogoro mpaka watu wanashindwa kulima na mvua imenyesha. Kama mmeshindwa kutatua migogoro mseme mmeshindwa nilete wengine. Haiwezekani nchi hii watu wanagombea mipaka tena wote ni watanzania wanazungumzia lugha moja,” amesema.

Rais Magufuli amesema kuwa, ni aibu kwaTaifa lililosifika kwa kutokuwa na migogoro ya ardhi kutokana na hekima za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, kuwa na migogoro hasa katika mkoa wa Mara aliotoka mwasisi huyo wa Taifa.

“Baba wa taifa alizuia migogoro mingi, taifa hili lilisifika kwa kutokuwa na migogoro mingi kutokana na hekima ya baba wa taifa, Ninawaomba msimwaibishe baba wa taifa kwa kuwa na migogoro mingi.” Amesema na kuongeza.

“Mkoa huu migogoro ya ardhi imekuwa ni tatizo, migogoro kati ya vijiji na vijiji na mtu na mtu. Tusije kuwa na migogoro wakati tunaweza kuimaliza wenyewe. Haiwezekani kuwe na vijiji vina mgogoro ndani ya mkoa mmoja, inabidi tuimalize wenyewe.

“Tusiliingize taifa kwenye ,migogoro hiyo. Ninawaomba wakazi wa Butiama, Bunda na maeneo jirani msigombane, msisubiri viongozi wa nchi wa wilaya au mikoa watatulie migogoro yenu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Afya ya akili yatajwa chanzo kuvunjika ndoa

Spread the loveCHANGAMOTO ya afya ya akili, imetajwa kuwa chanzo cha migogoro...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!