Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli awashangaa wabunge wa upinzani wanaohamia CCM
Habari za Siasa

Rais Magufuli awashangaa wabunge wa upinzani wanaohamia CCM

Mwenyekiti wa CCM, John Magufuli
Spread the love

HUKU vikao cha Chama cha Mapinduzi (CCM) vikiendelea, Mwenyekiti wa chama hicho, John Magufuli, ameoneshwa kushtuka kwa wimbi la wapinzani wanaotoka katika vyama vya upinzania na kuhamia CCM, anaandika Dany Tibason.

Akizungumza na wajumbe wa mkutano wa CCM Magufuli amesema kuwa kuna kila sababu ya kuwatafakari wale ambao wanataka kuhamia CCM kwa madai kuwa uenda wakawa wametumwa kuvuruga chama hicho.

Amesema kuwa inashangaza kuona mbunge ambaye analipwa zaidi ya Sh. 12 milioni kwa mwezi anaachia mshahara wake na kujiunga na CCM jambo ambalo amesema kuwa linatia shaka

Hata hivyo amesema kuwa mpaka sasa wapo baadhi ya wabunge wa upinzani takribani 10 na madiwani saba wameomba kujiunga na CCM lakini bado wameambiwa waendelee na ubunge wao hadi watakapo kuwa wamemaliza.

Hata hivyo wajumbe wa mkutano huo waliokuwa wakizungumza na mwenyekii wao walipaza sauti wakimtaka mwenyekiti kuakubalia wabunge hao waotoka upinzani wajiunge na CCM kwa madai kuwa watakuwa wamepunguza nguvu za upinzani.

Hata hivyo wachambuzi wa masuala ya kisiasa wamesema kuwa kinachofanywa na CCM kwa sasa ni kutaka kudhoofisha nguvu ya upinzani jambo ambalo ni hatari katika masuala mazima ya demokrasia.

Wakizungumza na MwanaHALISI Online kwa mashariti ya kutokutajwa majina walitaka ofisi ya spika ieleze wabunge ambao wamekuwa wakiachia ngazi na kwa wale ambao wamekuwa na mikopo hiyo mikopo inalipwaje na mpaka sasa ni wabunge wangapi wamerejesha mikopo na asiporejesha zitachukuliwa hatua gani.

Hata hivyo Mwenyekiti wa CCM taifa amekiri kutumia sera za wapinzani katika kutekeleza matakwa ya wananchi huku akiwataka wanachama wao kwa sasa wana mikakati gani kwani kwa sasa kinachotekelezwa ni ilani ya wapinzani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!