Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli awapa zawadi wafungwa
Habari za SiasaSiasa

Rais Magufuli awapa zawadi wafungwa

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli leo tarehe 16 Julai 2019, ametoa zawadi ya magunia 15 ya mchele pamoja na ng’ombe watatu kwa wafungwa na mahabusu waliopo kwenye gereza kuu la Butimba, jijini Mwanza. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kiongozi huyo wa nchi yupo ziarani jijini Mwanza ambapo ametembelea gereza hilo. Hata hivyo, mahabusu hao walipata fursa ya kumweleza Rais Magufuli changamoto wanazokumbana nazo.

“Hapa (gerezani) ni kama mtakuja, mimi ni kama mfungwa mtarajiwa, uongo?” aliwahoji wafungwa na mahabusu aliowatembelea.

Baada ya kuwauliza wanakula kiasi gani kwa wiki, Rais Magufuli aliwaeleza wakuu wa gereza hilo kuwa atawapelekea ng’ombe watatu na magunia 15.

“Sasa siku hiyo chinjeni ng’ombe na mpike mle. Ni nyinyi askari pamoja na hawa vijana, kula pamoja kunajenga upendo,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!