Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Michezo Rais Magufuli awapa moyo Taifa Stars, akubali mziki wa Senegal
Michezo

Rais Magufuli awapa moyo Taifa Stars, akubali mziki wa Senegal

Spread the love

RAIS John Magufuli amewapa moyo wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kufuatia kupoteza mchezo wao wa kwanza katika Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2019 nchini Misri dhidi ya Segenal kwa mabao 2-0, kuwa walifungwa na timu bora. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo tarehe 25 Juni 2019, Rais Magufuli amemtuma Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam anayetarajiwa kuelekea Misri kushuhudia michuano hiyo, kuwafikishia salamu zake wachezaji hao ya kwamba wasikate tamaa.

Rais Magufuli amesema licha ya Taifa Stars kupigwa mabao 2-0 na Senegal, wamepata mwanzo mzuri kutokana na timu hiyo kusheheni wachezaji wa kimataifa na kuongoza kwa ubora barani Afrika.

“Na mimi nina uhakika hata huo mwanzo siyo mbaya sana, kufungwa tugoli tuwili tu, kwa timu ambayo inaongoza katika Afrika ambayo wachezaji wote wanacheza nje, mimi ninafikiri tuwape moyo,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli amewataka wachezaji wa Taifa Stars kujituma katika michuano hiyo ili ipate matokeo mazuri yatakayowawezesha kusonga mbele, huku akiwataka Watanzania kuiombea timu yao ili ipate mafanikio.

“Ninakuruhusu nenda (Makonda) si umesema ukienda tutashinda? Basi nenda kwa sababu sisi sote tunataka kushinda, ukawaambie wachezaji wasikate tamaa. Kwenye mpira kuna kushinda, kushindwa na kutoka sare. Wao wakazane wakajitume zaidi na si tuendelee kuwaombea kwa sababu kushindwa kwao ni kushindwa kwetu,” amesema Rais Magufuli.

Taifa Stars itacheza mchezo wake wa pili wa Kundi C katika michuano hiyo siku ya Alhamisi ya tarehe 27 Juni mwaka huu, dhidi ya Kenya kabla ya kumaliza mchezo wa hatua ya makundi dhidi ya Algeria tarehe 1 Julai, 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!