Monday , 29 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli awaapisha Mawaziri, Manaibu wapya
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli awaapisha Mawaziri, Manaibu wapya

Rais John Magufuli
Spread the love

JOHN Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania muda mchache uliopita amewaapisha mawaziri wawili na manaibu wanne aliowateua siku ya Jumamosi tarehe 10 Novemba, 2018 kutokana na mabadiliko madogo aliyoyafanya katika baraza la mawaziri. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Waziri wa kwanza kuapa alikuwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Joseph Kakunda na kufuatiwa na Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga.

Baada ya mawaziri hao walifuatia manaibu waziri ambao ni Mary Mwanjelwa (ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma), Costantine Kanyasu (Maliasili na Utalii), Innocent Bashungwa (Kilimo) na hatimaye Mwita Waitara (Tamisemi)

Mbali na mawaziri na manaibu pia ameapishwa Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha sheria Jaji Januari Msofe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

error: Content is protected !!