RAIS John Pombe Magufuli ameivunja bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Ikulu, Gerson Msigwa inasema Rais Magufuli ameivunja bodi hiyo leo Jumapili tarehe 23 Septemba, 2018.
Bodi hiyo iliyokuwa inaongozwa na Mwenyekiti wake, Brigedia Generali mstaafu Mhandisi Mabula Mashauri imevunjwa wakati Kamati maalum ya Uchunguzi wa ajali ya MV Nyerere iliyotokea Septemba 20 ikianza kazi ya kuchunguza tukio hilo lililopoteza uhai wa watu zaidi ya 200.
Leave a comment