Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli aula SADC
Habari za Siasa

Rais Magufuli aula SADC

Rais John Magufuli
Spread the love

DK. John Magufuli, Rais wa Tanzania ameteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo tarehe 18 Agosti, 2018 na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Rais Magufuli ameteuliwa na Wajumbe walioshiriki katika mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC uliofanyika Windhoek nchini Namibia kuanzia tarehe 17 hadi 18 Agosti mwaka huu.

Rais Magufuli atashikilia wadhifa huo kuanzia mwezi Agosti 2018 mpaka Agosti 2019.

Kufuatia uteuzi huo, Dk. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atapewa rasmi jukumu la Uenyekiti wa SADC katika Mkutano mkuu ujao wa 39 utakaofanyika Tanzania mwezi Agosti 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!