Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi kwa Kenyatta
Habari Mchanganyiko

Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi kwa Kenyatta

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli ametuma salamu za pole kwa Rais wa Jamhuri ya Kenya, Uhuru Kenyatta kufuatia shambulizi la kigaidi lililopoteza maisha ya watu 21. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Tukio hilo ambalo linatajwa kutekelezwa na kundi la kigaidi la Al-Shabaab, lilitokea katika hoteli ya DusitD2 iliyoko jijini Nairobi tarehe 15 Januari 2019, ambapo hadi sasa taarifa zinaeleza kuwa, watu 28 wamejeruhiwa huku wengine 19 wakipotea kusikojulikana.

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter, Rais Magufuli amempa pole Rais Kenyatta kwa kuandika kuwa, “Punde nimezungumza na Mhe. Kenyatta kuhusu shambulizi la Jijini Nairobi, zaidi ya watu 14 wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa. Pole sana Mhe. Rais na pole sana wananchi wa Kenya. Tupo nanyi katika kipindi hiki cha majonzi. Nawaombea Marehemu wote walale mahali pema peponi, Amina.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi wa wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Spread the love  KAMISHNA wa Polisi Utawala Menejimenti ya rasilimali watu, CP...

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!