Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari Rais Magufuli ateua RC, Katibu mkuu na DC Dodoma
Habari

Rais Magufuli ateua RC, Katibu mkuu na DC Dodoma

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali kama ifuatavyo akiwemo mkuu wa mkoa (RC), katibu mkuu na mkuu wa wilaya (DC). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa iliyotolewa leo Ijumaa tarehe 17 Julai 2020 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema wateuliwa wote wataapishwa Jumatatu tarehe 20 Julai 2020 Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.

Walioteuliwa, Kwanza, Rais Magufuli amemteua Dk. Jumanne Fhika kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe.

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Fhika alikuwa Ofisi ya Rais na anachukua nafasi ya Christopher Ole Sendeka.

Pili, Rais Magufuli amemteua Dk. Aloyce Nzuki kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii.

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Nzuki alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii na anachukua nafasi ya Profesa Adolf Mkenda.

Tatu, Rais Magufuli amemteua Mhandisi Anthony Sanga kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji.

Kabla ya uteuzi huo, Mhandisi Sanga alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na anachukua nafasi ya Profesa Kitila Alexander Mkumbo.

Soma zaidi hapa

Rais Magufuli awaapisha warithi wa Makonda, Mnyeti

Nne, Rais Magufuli amemteua Dk. Allan Kijazi kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii.

Dk. Kijazi anachukua nafasi ya Dk. Aloyce Nzuki aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, na pia Dk. Allan Kijazi ataendelea kuwa Kamishna wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA).

Tano, Rais Magufuli amemteua Mhandisi Nadhifa Kemikimba kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji.

Kabla ya uteuzi huo, Mhandisi Nadhifa Kemikimba alikuwa Mkurugenzi katika Wizara ya Maji na anachukua nafasi ya Mhandisi Anthony Sanga ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji.

Soma zaidi hapa

JPM: Sijamtuma mtu akagombee, awapa ujumbe wanaCCM

Sita, Rais Magufuli amemteua Fadhili Mohamed Juma kuwa Mkuu wa Wilaya ya Geita Mkoani Geita.

Kabla ya uteuzi huo, Fadhili Mohamed Juma alikuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Lindi na anachukua nafasi ya Josephat Paulo Maganga ambaye amehamishwa kituo cha kazi na kuwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma.

Josephat Paulo Maganga anachukua nafasi ya Patrobas Katambi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!