KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, Rais John Magufuli ameondoa amri ya kuwazuia wananchi kulima katika maeneo ya mito na kuwataka kuendelea kufanya hivyo hata kama maji yatasomba maza yao, anaandika Richard Makore.
Ametoa agizo hilo leo eneo la Kyaka mkoani Kagera katika ziara yake na kusema kwamba wananchi waachwe walime mahali popote hata kama ni kwenye mito.
Agizo hilo limekuja baada ya Rais Magufuli kusimamishwa na wananchi njiani huku mmoja wao akiibuka na kulalamika vijana kuzuiwa kulima na kufanya biashara katika maeneo yaliyo karibu na mito.
Mara kadhaa serikali kupitia kwa wakuu wa Wilaya na viongozi wengine wamekuwa wakiwazuia wananchi kulima ama kufanya shughuli jirani na vyanzo vya maji ikiwamo mito kwa kuwa wanahataraisha kukausha maji.
TAARIFA KAMILI ANAGALIA VIDEO HII
Leave a comment