Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli arudi nyumbani Chato, afurahia maendeleo
Habari za Siasa

Rais Magufuli arudi nyumbani Chato, afurahia maendeleo

Rais John Magufuli alipowasili nyumbani kwao Chato
Spread the love

RAIS John Magufuli ameeleza kufurahishwa kwake na maendeleo yaliyofikiwa na wananchi wa Wilaya ya Chato mkoani Geita. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza baada ya kuwasili wilayani humo leo tarehe 1 Julai 2019, Rais Magufuli amewapongeza wananchi wa Chato kwa maendeleo wanayopata kutokana na jitihada zao za utendaji kazi.

Rais Magufuli amewahimiza wananchi hao kuongeza juhudi na maarifa katika utekelezaji wa majukumu yao.

“Nawapongeza sana wananchi wa Chato, mnachapa kazi kwelikweli na maendeleo yanaonekana, Chato inabadilika. Nilishasema asiyefanya kazi na asile, kwa hiyo tuendelee kushikamana kufanya kazi na kujenga nchi yetu,”amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli amewasili katika kijiji cha Mlimani wilayani Chato, kwa ajili ya mapumziko.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!