Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli aonya wanasiasa
Habari za Siasa

Rais Magufuli aonya wanasiasa

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli, Amiri Jeshi Mkuu wa Nchi, ameonya wanasiasa wanaodhalilisha vyombo vya ulinzi na usalama nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa nyumba za polisi mkoani Geita leo tarehe 15 Julai 2019, Rais Magufuli amewataka wanasiasa kujiepusha na tabia ya kutoa maneno yanayodhalilisha vyombo hivyo.

Ameeleza kuwa, wanasiasa hao hutoa maneno hayo kwa vyombo vya ulinzi  na usalama kwa ajili ya kutafuta sifa na umaarufu kwa wananchi.

“Nawasihi wanasiasa wenzetu tujiepushe na tabia ya kutoa maneno yanayodhalilisha vyombo vya ulinzi na usalama kwa lengo la kujitafutia sifa na umaarufu kwa wananchi,” amesema Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Rais Magufuli ameagiza Jeshi la Polisi kujipanga kwa ajili ya kusimamia uchaguzi wa serikali za kitaa unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

“Kusisitiza umuhimu wa jeshi kuendelea kujipanga katika kipindi ambacho nchi yetu inajiandaa na uchaguzi wa serikali za mitaa,” ameagiza Rais Magufuli.

Kuhusu uzinduzi wa nyumba hizo, Rais Magufuli ameipongeza Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi pamoja na Jeshi la Polisi kwa kufanikisha utekelezaji wa ujenzi wa nyumba hizo.

Aidha, ameliagiza Jeshi la Polisi kuhakikisha kwamba ujenzi wa nyumba unamalizika kwa wakati.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!