Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli ang’oa wakurugenzi wawili wa Halmashauri
Habari za Siasa

Rais Magufuli ang’oa wakurugenzi wawili wa Halmashauri

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli ametengua uteuzi wa Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe na Uyui mkoani Tabora. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Gerson Msigwa, inaeleza kwamba Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Adelius Makwega na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui, Hadija Makuwani.

Taarifa ya Msigwa inaeleza kuwa, Rais Magufuli ametangaza uamuzi huo leo tarehe 16 Mei 2019 katika kikao cha kazi, kati yake na Wakuu na Makatibu Tawala wa Mikoa, Makatibu na Wakuu wa Wilaya pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri za Majiji, Manispaa, Miji na Wilaya kilichofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.

“Wakurugenzi wa Halmashauri hizo watateuliwa baadaye,” inaeleza sehemu ya taarifa ya Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

error: Content is protected !!