Friday , 2 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli amtumbua Mkurugenzi
Habari za Siasa

Rais Magufuli amtumbua Mkurugenzi

Spread the love

RAIS John Magufuli ametengua uteuzi wa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa, Mohamed Maje kuanzia leo kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Akitoa taarifa ya utenguzi huo mjini Dodoma, Katibu Mkuu wa Tamisemi, Alhaji Mussa Iyombe amesema kuwa Maje ameisababishia serikali hasara ikiwemo kushindwa hata kukusanya mapato ya serikali.

Utenguzi wa Maje umetokana na taarifa iliyotolewa na tume iliyoundwa kukagua utendaji wake wa kazi nakubaini kuwa ameshindwa kusimamia na kudhibiti mapato ya halmashauri hali iliyopelekea upotevu wa fedha.

“Hadi kufikia robo tatu ya mwaka wa fedha halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa imekusanya mapato kwa asilimia 24 tu pamoja nakuwa halmashauri hiyo ni kongwe na yenye vyanzo vingi vya mapato,” amesema Iyombe.

Hatua hii imekuja baada ya Mkuu wa mkoa wa Dodoma Dk. Bilineth Mahenge kuagiza kuundwa kwa tume ya mkoa kuchunguza ubadhilifu wa fedha zaidi ya Sh. 500 milioni katika halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa pamoja na kubaini sababu za halmashauri hiyo kuwa ya mwisho katika ukusanyaji wa mapato.

Akizungumza katika kikao cha ushauri wa mkoa (RCC) Mahenge alionyesha kusikitishwa na matokeo hayo pamoja na kuwa wilaya Kongwe nayenye vyanzo vingi vya mapato kukusanya asilimia 24 pekee ya mapato hivyo kupelekea kuchukuliwa hatua kwa watendaji wote wanaokwamisha ukusanyaji wa mapato ya ndani.

Hata hivyo Mahenge alisisitiza uadilifu kwa watendaji ikiwa ni pamoja na kupeleka mashine za kukusanyia mapato katika kata.

“Ukusanyaji wa mapato ya ndani ni muhimu sana katika halmashauri kwani ndio hutumika katika shughuli za maendeleo,ukuaji na ustawi wa halmashauri,” amesema Mahenge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!