Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli akata ngebe za wanaoibeza Dreamliner
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli akata ngebe za wanaoibeza Dreamliner

Spread the love
RAIS John Magufuli amekata mzizi wa fitina kwa wanaoibeza ndege ya Dreamliner wakidai mbovu, baada ya kuamua kutumia ndege hiyo kwenda jijini Mwanza leo Jumamosi tarehe 18 Agosti, 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Katika safari hiyo Rais Magufuli alitumia kuzungumza na abiria waliopanda ndege hiyo ikiwa pamoja na kupiga nao picha mbalimbali kama kumbukumbu.

Ndege hiyo ilizua gumzo mitandaoni wiki iliyopita baada ya kusimamisha huduma kwa matengenezo ya kawaida kabla ya kuanza tena safari zake za kawaida za Dar es Salaam, Moshi na Mwanza.

Kitendo cha Rais Magufuli kutumia ndege hiyo kubwa zaidi nchini, ni kuwahakikishia wananchi kuwa ipo salama na wamezungumza na kuwapongeza wananchi waliosafiri nao pamoja.

Rais Magufuli baada ya kushuka uwanja wa Ndege wa Mwanza alikwenda katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando akapopokewa na viongozi kadhaa akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella.

Wakati akitoka katika hospitali hiyo alisimamisha msafara wake na kuzungumza na wanafunzi wa Shule Msingi Mongella iliyopo eneo la Bugando waliokuwa wamesimama pembeni mwa barabara.

“Mmekuja kufanya nini hapa,” Rais Magufuli aliwauliza swali wanafunzi hao. Kwa sauti ya pamoja, wanafunzi hao wakajibu “Tumekuja kukuona”

Baada ya jibu hilo, Rais Magufuli aliwashukuru wanafunzi hao na kuwaambia, “Nitarudi siku nyingine kuonana na kuzungumza nanyi. Leo nimefika hapa kumuona mgonjwa wangu ambaye amelazwa hapa hospitalini. Endeleeni kuwaombea wagonjwa waliolazwa hospitalini.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!