Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli afarika dunia
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli afarika dunia

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli, amefariki dunia jana Jumatano, tarehe 17 Machi 2021, saa 12:00, katika Hospitali ya Mzena, jijini Dar es Salaam, kwa maradhi ya moyo. Anaripoti Mwandishi Wetu.

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, akitangaza msiba huo mzito kwa Taifa, amesema, Rais Magufuli alianza kuumwa tatizo la mfumo wa umeme wa moyo tarehe 6 Machi 2021 na kutibiwa Hospital ya Moyo ya Jakaya Kikwete kisha kuruhusiwa 7 Machi 2021, kuendelea na majukumu yake.

Mama Samia amesema, tarehe 14 Machi 2021, hali yake ilibadilika na kupelekwa Hospital ya Mzena, Dar es Salaam hadi mauti yalipomfika.

Makamu huyo wa Rais, ametangaza siku 14 za maombolezo na bendera zitapepea nusu mlingoni huku taratibu zingine za mazishi zikiendelea.

Dk. John Pombe Joseph Magufuli alizaliwa tarehe 29 Oktoba 1959 huko wilayani Chato Mkoani Kagera (hivi sasa Chato ni wilaya ya mkoa mpya wa Geita).

Aliingia madarakani kama Rais kwa mara ya kwanza tarehe 5 Novemba 2015, akichukua nafasi iliyokuwa imeachwa wazi na Jakaya Mrisho Kikwete, aliyekua amemaliza muda wake wa utawala wa miaka kumi.

Dk. Magufuli, alifanikiwa kutetea nafasi hiyo tena katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka jana-2020 na kuapishwa tarehe 5 Novemba 2020, ili kuhitimisha miaka kumi ya utawala wake.

6 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!