RAIS John Magufuli amemteua Balozi Mstaafu, Ali Idi Siwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF). Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo tarehe 20 Septemba 2018 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa.
“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli amemteua Balozi Mstaafu Ali Idi Siwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Taarifa hiyo inaeleza kuwa, uteuzi wa Balozi Siwa unaanza leo.
Leave a comment