RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemteua Marwa Mwita Rubirya kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe (RC). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Uteuzi huo ni mabadiliko ya uteuzi alioufanya Rais Magufuli tarehe 17 Julai 2020 alipomteua Dk. Jumanne Fhika kuwa Mkuu wa Mkoa huo.
Kabla ya uteuzi huo, Dk. Fhika alikuwa Ofisi ya Rais na aliteuliwa kuchukua nafasi ya Christopher Ole Sendeka.
Hata hivyo, leo Jumapili tarehe 19 Julai 2020, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu ya Tanzania, Gerson Msigwa amesema Dk. Fhika atabaki Ofisi ya Rais kuendelea na majukumu yake.
Taarifa yote ya Msigwa hii hapa chini;
Leave a comment