Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais ‘Kiduku’ aibipu UN
Kimataifa

Rais ‘Kiduku’ aibipu UN

Spread the love

RAIS wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un maarufu kama ‘Kiduku’ kutokana na staili yake ya nywele, amesimamia urushwaji wa kombora la masafa mafupi kuelekea pwani ya Bahari ya Mashariki licha ya Umoja wa Mataifa kumuonya kuhusu harakati zake. Anaripoti Glory Massamu – TUDARCo… (endelea)

Jaribio hilo limefanyika mapema leo tarehe 28 Septemba 2021 ikiwa ni siku chache zimepita tangu Balozi wa taifa hilo, Kim Song kuhutubia mkutano wa Umoja wa Mataifa na kusisitiza kuwa nchi hiyo itaendelea kupima ubora wa silaha zake.

Akizungumza katika mkutano huo jijini New York unaofanyika kila mwaka, Balozi huyo wa Korea alisema hakuna mtu anayeweza kukataa haki ya nchi yake kujilinda na kujaribu silaha zake.

Awali Korea Kaskazini ilirusha makombora mapema mwezi huu jambo ambalo lililalamikiwa na majirani zao Japan ambao kupitia wizara ya ulinzi ilisema makombora yaliyorushwa yalikuwa ya masafa marefu wakati yamepigwa marufuku na UN.

Hata hivyo, Rais wa Korea Kusini, Moon Jae-in ameliagiza Baraza la Usalama la Taifa la nchi hiyo kuchambua na kufutilia malengo ya kurushwa kwa makombora hayo na kauli za hivi karibuni zilizotolewa na dada yake Rais wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un.

Dada huyo anayefahamika kwa jina la Kim Yo-jong alisema nia ya taifa lao ni kumaliza uhasama kati ya nchi hizo mbili yaani Korea Kusini na Kaskazini.

Korea Kaskazini mara kwa mara imekuwa ikiishutumu Korea Kusini kuhusu ya shughuli zake za kijeshi zinazofanywa na taifa hilo na kusema kua wanahitaji kujilinda na kujenga usalama na amani ya nchi.

Aidha, Marekani ilisema inafahamu kuhusu kombora hilo lakini pia imesema kitendo hicho kinaonyesha athari mbaya ya mpango wa silaha haramu wa Korea Kaskazini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!