Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Kenyatta atoa siku 14 mahindi kuondoka mpakani
Habari Mchanganyiko

Rais Kenyatta atoa siku 14 mahindi kuondoka mpakani

Spread the love

 

UHURU Kenyatta, Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, ametoa siku 14 kwa mawaziri wake, kuhakikisha mahindi kutoka Tanzania, yaliyokwama mpaka wa Namanga, mkoani Arusha yanaondoka. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Rais Kenyatta, ametoa agizo hilo, leo Jumatano, tarehe 5 Mei 2021, mbele ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, wakati akizungumza katika Jukwaa la Wafanyabiashara, kati ya Tanzania-Kenya.

Ni katika siku ya pili na ya mwisho ya ziara ya Rais Samia nchini Kenya, aliyoianza jana Jumanne na ataihitimisha leo Jumatano na kurejea nchini mwake Tanzania.

Agizo hilo, amelitoa ikiwa ni takribani miezi miwili, malori yenye shehena ya mahindi, yamekwama kwenye mpaka wa Namanga.

Ni baada ya Kenya, kupiga marufuku ununuzi wa mahindi kutoka mataifa jirani ya Tanzania na Uganda kutokana na kile kinachoelezwa kwamba mahindi kutoka nchi hizo mbili sio salama kwa matumizi ya binadamu.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya kilimo na chakula wa nchini Kenya wakati zuio hilo linatolewa, ilieleza mahindi hayo yana kiwango kikubwa cha sumu kuvu, ambayo ni hatari kwa usalama wa walaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!