Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Issoufou atunukiwa tuzo ya Mo Ibrahim
Kimataifa

Rais Issoufou atunukiwa tuzo ya Mo Ibrahim

Spread the love

MAHAMADOU Issoufou, Rais Mstaafu wa Niger, ametunukiwa tuzo ya Mo Ibrahimu inayoonesha Ufanisi katika Uongozi kwa Afrika. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Rais Issoufou aliteuliwa kutwaa tuzo hiyo baada ya kikao cha Kamati Huru ya Tuzo hiyo kukutana jana Jumatatu tarehe 8 Machi 2021.

Taarifa kutoka kwenye kamati hiyo imeeleza, miongoni mwa kilichoisukuma kumteua kiongozi huyo ni pamoja na kulisaidia taifa lake kiuchumi wakati wa utawala wake (2011-2020).

Rais Issoufou amekuwa kiongozi wa sita kupokea tuzo hiyo ya heshima Afrika kwa viongozi wastaafu wa mataifa yao.

Kiongozi huyo pia, amesifiwa na kamati hiyo kwa kuimarisha demokrasia sambamba na kulinda utawala wa sheria. Na kwamba, wakati akichukua, nchi hiyo ilikuwa katika uchumi duni.

Festus Mogae, mwenyekiti wa hamati hiyo ambaye ni Rais Mstaafu wa Botswana amesema, Rais Issoufou alisimama imara wakati nchi yake ikipita kwenye misimamo mikali ya vurugu, kuongezeka kwa jangwa pamoja na hali mbaya ya kisiasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Mpinzani mkuu wa Rais Kagame aachiwa huru

Spread the love  PAUL Rusesabagina, aliyewahi kuripotiwa kama ‘shujaa’ katika filamu ya...

Kimataifa

Rais Tshisekedi amteua kiongozi wa wanamgambo kuwa Waziri wa Ulinzi

Spread the love  RAIS wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Felix Tshisekedi,...

Kimataifa

Raila Odinga: Tutafanya maandamano makubwa mara mbili kwa wiki

Spread the love KIONGOZI wa upinzani nchini Kenya, Raila Amollo Odinga ametangaza...

Kimataifa

Magharibi kuwekeza silaha Indo-Pacific, China yachochea

Spread the love KUVUNJIKA ushirhikiano wa China na Magharibi uliodumu kwa takribani...

error: Content is protected !!