Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Congo: M23 bado wapo, wamedanganya
Kimataifa

Rais Congo: M23 bado wapo, wamedanganya

Felix Tshisekedi, Rais wa DR Congo
Spread the love

 

RAIS wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Felix Tshisekedi amesema waasi wa M23 bado hawajaondoka kikamilifu katika maeneo wanayoshikilia mashariki mwa DRC. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Rais Tshisekedi, amewashutumu wanamgambo hao kwa kudanganya makubaliano ya kuondoa vikosi vyake.

Viongozi wa kikanda walifikia makubaliano Novemba mwaka jana ambapo kundi hilo la Kitutsi lilipanga kujiondoa katika maeneo inayo shikilia ifikapo tarehe 15 Januari 2023.

Hiyo ilikuwa ni sehemu ya juhudi za kumaliza mgogoro ambao umewakosesha makazi watu 450,000 na kuzusha mgogoro wa kidiplomasia baina ya Congo na jirani yake Rwanda.

Akiwa Davos, Uswisi katika mkutano wa dunia wa uchumi Rais Tshisekedi, alisema licha ya msukumo wa kimataifa kundi hilo bado lipo katika maeneo hayo.

Ameongeza kusema kundi hilo linajifanya kuondoka lakini ukweli ni kwamba bado lipo katika maeneo inayoshikilia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!