Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Michezo Rais CAF aguswa na ajali ya MV Nyerere
Michezo

Rais CAF aguswa na ajali ya MV Nyerere

Spread the love

RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Ahmad Ahmad kupitia Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia ametuma salamu za rambirambi msiba wa waliofariki kwenye ajali ya kivuko cha MV Nyerere kilichozama juzi kati ya Ukara na Bugorara, Ukerewe. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Rais wa CAF, Ndugu Ahmad ametoa pole kwa Rais wa Tanzania, Dk. John Magufuli na watanzania kiujumla na pia ametoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki kwa msiba huo mzito uliosababisha majonzi makubwa kwa Watanzania.

“Naungana na Watanzania na Rais wa Tanzania, John Magufuli kwa msiba huo mzito kwa Tanzania,” alisema Rais wa CAF.

Wakati huohuo, Karia kwa niaba ya TFF ametoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa waliofariki katika ajali hiyo.

Karia amesema ni huzuni kubwa kwa Taifa na Watanzania kwa ajali hiyo iliyopoteza wapendwa wetu.

Amesema ajali hiyo imepoteza wana familia ya Mpira wa miguu ambao walikuwa wakifuafilia ama mashabiki wa mchezo huo lakini pia ajali hiyo imepoteza nguvu kazi ya Taifa.

TFF inaungana na Ndugu, jamaa na marafiki katika kipindi hiki kigumu cha kupoteza wapendwa wao. Pia inawapa pole na kuwatakia afya njema majeruhi waliookolewa katika ajali hiyo iliyotokea jana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMichezo

Mwana FA anogesha Tamasha la Exim Bima Festival

Spread the loveNAIBU Waziri Wa Utamaduni, Sanaa Na Michezo, Hamis Mwinjuma ‘Mwana...

Michezo

Manchester City dhidi ya Tottenham ni usiku wa kisasi

Spread the love KIPUTE kati ya klabu ya Manchester City dhidi yaTottenham Hotspurs...

Michezo

Wikiendi ya kutamba na Meridianbet hii hapa usikubali kuikosa

Spread the loveMERIDIANBET wanakwenda kukupa nafasi ya kutambawikiendi hii kupitia ODDS KUBWA walizoweka...

Michezo

Fernandes hakamatiki Man Utd, mahesabu ni kuifunga Bayern

Spread the love  NAHODHA wa Manchester United, Bruno Fernandes, alikuwa na kiwango...

error: Content is protected !!