Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari Rais AfDB azuru kaburi la Hayati Magufuli
HabariTangulizi

Rais AfDB azuru kaburi la Hayati Magufuli

Spread the love

RAIS wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Daktari Akinwumi Adesina, amezuru katika kaburi la aliyekuwa Rais wa Tanzania wa Awamu ya Tano, Hayati John Magufuli, lililoko wilayani Chato, Mkoa wa Geita. Anaripoti Mwandishi Wetu, Geita…(endelea).

Dk. Adesina amelitembelea kaburi hilo jana tarehe 10 Februari 2022, katika ziara yake ya siku moja yenye lengo la kutoa salamu za pole kwa familia ya Hayati Magufuli, ambapo alipokelewa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Chato, Wilson Shimo.

Rais huyo wa AfDB alisema ziara yake hiyo inatokana na urafiki mkubwa, kati yake na Hayati Magufuli.

“Rais Magufuli alikuwa mfano mzuri kwa viongozi barani Afrika, aliwapenda Watanzania na Waafrika wote, kwa moyo wake wote,” alisema Dk. Adesina.

Dk. Adesina alimshukuru Rais Samia kwa kumruhusu yeye na ujumbe wake kuzuru katika kaburi hilo, huku akisema Tanzania iko kwenye mikono salama chini yake, ambaye anaendeleza mazuri yaliyoachwa na Hayati Magufuli.

Hayati Magufuli aliyeiongoza Tanzania kwa miaka mitano na miezi kadhaa mfululizo (2015 hadi 2021), alifariki dunia tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Makumbusho jijini Dar es Salaam, alikokuwa anapatiwa matibabu ya ugonjwa wa mfumo wa umeme wa moyo.

Mwili wake ulizikwa kijijini kwao Chato mkoani Geita, tarehe 26 Machi mwaka jana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!