Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Addo amwibia Clinton, Bush
Kimataifa

Rais Addo amwibia Clinton, Bush

Spread the love

AKIWA na siku tatu ndani ya Ikulu ya Ghana, Rais Nana Akufo Addo anatuhumiwa kuiba sehemu ya hotuba za marais wa Marekani siku ya kuapishwa kwake jijini Accra, anaandika Wolfram Mwalongo.

Mitandao ya kijamii ya nchini humo imemshambulia rais hiyo kwa kunyofoa maneno kwenye hotuba zilizotolewa na aliyekuwa rais wa 42 wa Marekani, Bill Clinton aliyoitoa mwaka 1993 pia Rais wa 43 George Bush aliyoitoa mwaka 2001.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Rais huyo amekiri kuchotwa kwa baadhi ya maneno kutoka katika hotuba za marais hao wa Marekani.

Ofisi hiyo imeomba radhi kwa umma kutokana na kitendo hicho kilichoanza kuibua mijadala katika mitandao ya kijamii tangu siku ya kuapishwa kwake.

Tukio la aina hii lilitokea mwaka jana katika kampeni za uchaguzi mkuu wa Marekani baada ya Melania Trump, mke wa Donald Trump alipotoa hotuba tarehe 19 Juni mwaka jana iliyofanana na ile iliyotolewa na mke wa Barrack Obama, Michele Obama mwaka 2008. Melania alishambuliwana wafuasi wa Hillary Clinton.

Rais Addo aliapishwa tarehe 7 Januari mwaka huu baada ya kumwangusha John Mahama, rais aliyekuwa madarakani.

Katika hotuba yake aliyoitaoa Rais Addo ameahidi kuinua uchumi wa Ghana kwa kukuza biashara, kuongeza ajira.

Pia ameahidi kutokomeza umaskini katika taifa hilo huku akiwataka raia wa taifa hilo kushirikiana katika kutekeleza azma ya kuleta maendeleo ya taifa hilo.

“Nawaomba tuwe raia ambao sio watazamaji, raia tusiwe wa mameno, wajibu wa raia ni kujenga jamii yake na kuliletea maendeleo taifa lake. Tufanye kazi hadi pale tutakapoona kazi zimekwisha” amesema Rais Addo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!